Pages

Friday, 2 August 2013


Mugabe ‘amburuta’ Tsvangirai

 
0
Share

Mugabe ameiongoza Zimbabwe kwa miaka 33 wakati mpinzani wake aliyekuwa Waziri Mkuu anawania urais kwa mara ya tatu.
Vyama vinavyochuana ni pamoja na Zanu-PF cha Mugabe, MDC kilichomsimamisha Tsvangirai. Vingine ni Independent, UPP na Zapu.

Endelea...
Vyanzo mbalimbali vya habari vinaonyesha kuwa Mugabe amemwacha mpinzani wake kwa asilimia nyingi na zaidi katika jiji la Harare na Bulawayo.
Mugabe atamba
Akizungumza kwa kujiamini huku akiwa na wafuasi wake kadhaa, Mugabe alisema ana uhakika wa kupata ushindi wa kishindo.
Aliliambia Shirika la Habari la Uingereza (Reuters): “Sioni sababu ya kunifanya niwe na wasiwasi… hakuna kitakachonifanya nishindwe katika uchaguzi huu.”
Hata hivyo, Mugabe aliyeiongoza Zimbabwe tangu uhuru 1980, alisema iwapo atashindwa, yuko tayari kukabidhi madaraka kwa amani… “Ninaweza kustaafu baada ya kuwa madarakani kwa miaka 33 iwapo nitashindwa katika uchaguzi huu,” alisema.
Akizungumza baada ya kupiga kura juzi, Mugabe alisema ana uhakika kwamba uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki, kwa kuwa wagombea wote walipewa nafasi ya kutosha kufanya kampeni na wananchi kushiriki katika uchaguzi huo.
Alipoulizwa iwapo ana shaka yoyote kuhusiana na matokeo, alicheka kwa kejeli na kusema hawezi kuwa na hofu katika mambo ambayo amekutana nayo kwenye maisha yake na kuyashinda, akiwa na umri wa miaka 89 sasa.
Kumekuwa na taarifa zisizo rasmi kwamba iwapo Mugabe atashinda, anatarajia kustaafu kabla ya sherehe yake ya miaka 90 ya kuzaliwa na kumwachia madaraka mshirika wake ndani ya Zanu-PF.
Lakini alipoulizwa iwapo ataweza kuhudumu kwa kipindi cha miaka mitano, alisema: “Kwa nini isiwe? Hamtaki nihudumu kwa kipindi chote? Kwa nini nijitolee kuwa mgombea kwa ajili ya kuwadanganya watu kama nisingekuwa na mpango wa kuwatumikia?”

No comments: