Pages

Thursday, 15 August 2013

KERO YA MAJI YAWATESA WANANCHI WA KIJIJI CHA NJELENJE MBEYA

 
Na Esther Macha,wa matukiodaima.com  mbeya
WANANCHI wa Kata ya Mshewe  kijiji cha Njelenje Wilaya ya Mbeya wamelalamikia  kutokuwa na maji kwa muda wa miaka 10 licha  ya uongozi wa kata hiyo kuendelea kuwachangisha michango  ya mabomba wananchi hao .
Na Meck
endelea....
Wamesema ni jambo la kusikitisha kuona uongozi  uliopo kufanya kazi ya kuchangisha michango tangu mwaka 2009 mpaka sasa  na dalili za kuwepo maji hakuna na hata kusomewa mapato na matumizi ya fedha hizo hayapo.
Uchunguzi uliofanywa na Mtandao huu kwa kushirikiana na Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) umebaini kuwa maji ambayo wanatumia wananchi wa kijiji hicho ni yale ambayo yanatoka kwenye chanzo ambacho ni makaburi ya watu ambayo hata hivvyo hayana usalama wowote.
Hata hivyo  majira ilibaini kuwa maji hayo ambayo yapo kwen ye chem chem.  Makaburi  makazi yua watu ambako kuna vyoo kwa ujumla yanahatarisha  afya za wananchi wa eneo hilo hususan watoto wadogo.
Mmoja wa wananchi wa Kijiji cha  Njelenje Bw.Rashid Odati alisema  kuwa  toka wameanza kuchangia maji ni muda mrefu, kwani maji yaliyopo ambayo wanatumia  ni hatari kwa afya za wananchi kutokana na maji wanayotumia kutoka kwenye  chanzo ambacho kipo karibu na vyoo na makaburi ya watu.
“Hapa tulipo hatuelewi hatima yetu ni nini kwani maji tunayotumnia ni hatari sana kwa afya zetu hebu ndugu mwandishi wa habari angalia hicho chanzo kipo kati kati ya makaburi  kwa hali hii sidhani kama kuna uhakika wa sisi wananchi kupata maradhi”alisema Mkazi huyo.
Akizungumzia kuhusu viongozi alisema wamekuwa na sababu nyingi za kutoa kwa wananchi ambazo hazina umuhimu wowote kutoka kwa wananchi kwani  fedha ambazop zinachangwa na zimekuwa kama mtaji kwao wa kuendeshea maisha yao.
“Mfano huyu diwani wetu  amekuwa na amri zake kwa wananchi  kwa kutumia cheo chake  kukandamiza wananchi ,sisi hatutaki diwani awe mwiba kwetu kwa kutumia  nafasi yake  kama fimbo kwa wananchi “alisema Bw. Odati.
Mkazi mwingine Bi.Teddy Mwakaje alisema kutokana na shida ya maji hakuna maendeleo yeyote ambayo wanafanya kutokana na muda mwingi kutumia kutafuta maji kwani hata  yaliyopo kwenye chazo nayoi bado ni tatizo kuyapata licha ya kutokuwa na usalama wa  kutosha.
Akizungumzia tatizo hilo la maji Mwenyekiti wa kitongoji cha  Kizota  Bw. John Kapange alisema kuwa kero hiyo ya maji ni ya muda mrefu katika kijiji  hicho na kusababisha wananchi kutoka usiku wa manane kwenda kutafuta maji kwenye visima.
Akijibu malalamiko hayo ya wananchi  Diwani wa  Kata ya Mshewe Bw.Fabian  Mwakasole  alisema tatizo hilo la maji katika  kijiji cha Njelenje ni la muda mrefu na kwamba toka anaingia madarakani mwaka 2010 amelikuta.

No comments: