Pages

Sunday, 8 September 2013

Makubwa zaidi yafichuka dawa za kulevya

Mhadhiri na Mtaalamu wa Saikolojia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Kitila Mkumbo 
Kwa ufupi
Kwa yule ambaye si mzoefu wa kutumia vilevi hivi huwezi kuuziwa, kwani kuna ishara ambazo hupeana ili kujua kama huyu ni mnunuaji au polisi.

Mitaani vijana wanasikika wakisifia bangi inayouzwa na Khamis (siyo jina lake halisi). Wanashawishiana kwenda kununua kwa mtu huyo wakisifu kuwa ina ‘stimu’ nzuri isiyokwisha haraka tofauti na za mtu mwingine (wanamtaja kwa jina).
Kwa yule ambaye si mzoefu wa kutumia vilevi hivi huwezi kuuziwa, kwani kuna ishara ambazo hupeana ili kujua kama huyu ni mnunuaji au polisi.
Zipo ishara mbalimbali wanazozitumia wakati wa kununua bangi hizi, mfano ukiwa na gari usiku utatakiwa kuzima taa za nje na kuwasha za ndani. Muuzaji akiona hivyo tu anajua kuwa aliyefika ni mteja wake.
Aidha hata namna wanavyopeana pesa ni tofauti, muuzaji hakabidhiwi mkononi badala yake unaiweka tu kwenye kiti cha gari, naye akifika anaweka mzigo chini na kuchukua pesa yake.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umegundua kuwa, huu ndiyo mwanzo wa watumiaji wa bagi kuingia katika matumizi ya dawa za kulevya.
Aidha hata namna wanavyopeana pesa ni tofauti, muuzaji hakabidhiwi mkononi badala yake unaiweka tu kwenye kiti cha gari, naye akifika anaweka mzigo chini na kuchukua pesa yake.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umegundua kuwa, huu ndiyo mwanzo wa watumiaji wa bangi kuingia katika matumizi ya dawa za kulevya.
Wauza dawa za kulevya matajiri nchini, wanafanya hila kuhakikisha vijana wadogo wanaingia kwenye utumiaji wa dawa za kulevya, ili watengeneze wateja endelevu wa biashara yao.
Inasemekana kuwa kauli mbiu wanayoitumia ni ‘Get Them While They’re Young’, wakimaanisha kuwa wawaingize kwenye matumizi ya dawa za kulevya wakati wakiwa bado wadogo, ili wanapofikia umri wa kuingiza kipato wawafaidishe wao kwa kununua ‘unga’.
Uchunguzi unaonyesha kuwa matajiri hawa wakati mwingine huwalipa wauza bangi na kuwapa dawa za kulevya bure, ili wazichanganye wakiamini kuwa wanatengeneza wateja wengi kwa wakati mmoja.
Kwa wasiovuta bangi wamekuwa wakichanganyiwa katika sigara na matendo kama haya hufanyika zaidi katika klabu za usiku na waathirika wakubwa wa njia hii ni wasichana.
“Wasichana hudanganywa na wapenzi wao wakiambiwa vuta kidogo, ni nzuri nao hujikuta wakijaribu na kurudia tena kwa kuwa kile wanachovuta si sigara ya kawaida, mwisho wa siku huingia kwenye ‘uteja’” kinasema chanzo cha habari.

No comments: