WAHIMIZWA KUHUBIRI AMANI,UPENDO
Nzigilwa alisema viongozi wa dini wana mchango
mkubwa katika jamii, hivyo wanapaswa kuilinda na kuidumisha amani
iliyopo na kwamba jukumu walilonalo mapadri hao wapya ni kuhakikisha
jamii wanayoizunguka inaishi katika mazingira ya utulivu na amani kama
ndugu.
“Nendeni mkahubiri amani, furaha na upendo kwa watu wote hiyo ndiyo kazi yenu kubwa, tunahitaji kuwa na amani,” alisema Nzigela.
Akitoa neno la shukrani baada ya kupandishwa
daraja la upadri, Padri Siriack Malasi alisema kuwa safari ya kufikia
hatua hiyo haikuwa rahisi na kwamba wana kila sababu ya kuwashukuru watu
wote waliowawezesha kufika katika daraja hilo.
“Neno tunaloweza kulisema ni asante sana, tumepita
katika wakati mgumu na mara nyingine tulikuwa tunawasumbua kidogo. Hata
kufika kwenu hapa ni mchango muhimu, kama wangefika mapadri na maaskofu
bila nyinyi (waumini) ingekuwaje?” alihoji Malasi.
Misa hiyo ya upadrisho iliambatana na uzinduzi wa
kitabu cha marehemu Jackson Mosha aliyekuwa Mjasuiti ambaye alifariki
dunia mwaka 2009.
No comments:
Post a Comment