Pages

Tuesday, 15 October 2013

Hali ya muandishi wa habari wa ITV na Radio One Ufoo Saro inaendelea vizuri.

Hali ya muandishi wa habari wa ITV na Radio One Ufoo Saro aliyejaruhiwa kwa risasi na mzazi mwenzie inaendelea vizuri lakini bado yupo chini ya uangalizi maalum wa madaktari.

Kwa mujibu wa madaktari waliomfanyia upasuaji wa kuondosha risasi iliyokuwa tumboni Ufoo anahitaji muda mwingi wa kupumzika ili aweze kupata nafuu na kurudi katika hali yake ya kawaidia.



Muandishi huyo alipelekwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili akitokea Hospitali ya Tumbi Kibaha Mkoani Pwani ambapo alipelekwa mara baada ya kukutwa na tukio hilo.

Wednesday, 9 October 2013

Wawekezaji wanyanyasaji kufukuzwa


SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema wawekezaji watakaobainika kujishughulisha na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia pamoja na kuwasumbua wafanyakazi katika sekta za mahoteli watachukuliwa hatua za kinidhamu ikiwemo kufukuzwa nchini.

Mfanyabiashara Arusha adai kumwagiwa tindikali


MFANYABIASHARA Japhet Minja amelazwa katika Hospitali ya Arusha Lutheran Centre (Seliani) jijini Arusha, baada ya kumwagiwa kimiminika kinachosadikiwa kuwa tindikali usoni na watu wasiojulikana.

Vurugu mgomo wa mabasi na malori

MGOMO wa malori na mabasi kupinga Sheria ya Barabara inayowataka wasiongeze mizigo kupita kiwango cha mwisho cha uzito, umeingia katika sura nyingine ambapo baadhi ya wasemaji wa wamiliki, wamewasingizia viongozi kuwa wamelegeza msimamo.

Mazishi ya kitaifa kwa wahamiaji Lampedusa

zzzzlampedusa_cuerpos_italia_304x171_reuters_nocredit_a7059.jpg
Serikali ya Utaliana itafanya mazishi ya kitaifa kwa mamia ya wahamiaji waliokufa maji baada ya boti walimokuwa wanasafiria kuzama katika bahari ya Meditarenia kisiwani Lampedusa wiki iliyopita.