Pages

Tuesday, 23 July 2013

WAZEE 292 WAPATIWA VITAMBULISHO VYA MATIBABU

Kushoto ni Afisa mtendaji kata ya Utengule Usongwe wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani MBEYA,  John Mwanampazi, akiwa na Afisa Maendeleo ya Jamii kata hiyo Martin Gowele wakizungumza na mwandishi wa habari.


Kitambulicho cha matibabu kwa wazee waliofikisha miaka 60 na zaidi.
Na, Kelvin Lameck, Mbalizi

Endelea....

Ili kutekeleza sera ya taifa ya wazee ya mwaka 2003 inayosema wazee kuanzia miaka 60 watapata huduma za afya bure, Halmashauri ya wilaya ya Mbeya Vijijini, imeanza kuwapatia wazee vitambulisho vya kudumu vya matibabu.


Katika kata ya Utengule Usongwe yenye vijiji sita, wazee 292 tayari wamepatiwa vitambulisho hivyo ambavyo vitawawezesha kutibiwa bure maisha yao yote katika hospitali za serikali ndani ya mkoa wa Mbeya.


Wakizungumza na Mtandao wa Meck lameck.blogspot.com ofisini kwao, Ofisa mtendaji wa kata hiyo John Mwanampazi na ofisa Maendeleo ya jamii wa kata Martin Gowele, walisema kuwa awamu ya kwanza waliwapatia wazee192 na awamu ya pili wazee 80.


‘’Tuliwatangazia viongozi wa serikali za vijiji kuwa wazee wote wenye umri wa kuanzia miaka 60 wanapaswa kuleta picha moja ya Passport ambapo anatengenezewa kitambulisho cha matibabu’’ alisema Gowele.


Alisema wazee wengi wamejitokeza na baadhi wameanza kufurahia matibabu wanayopata bure kupitia vitambulisho hivyo.


Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji wa kata hiyo John Mwanampazi, alisema kijiji kinachoongoza kwa wazee wengi kujitokeza kupatiwa vitambulisho hivyo ni Kijiji cha Mbalizi.


‘’Mbalizi inaongoza na ninawataka wazee wote wenye kuanzia miaka 60 wajitokeze kuja kujiandikisha na kuchukua vitambulisho vya matibabu maana ni mpango wa serikali na vinatolewa bure’’ alisema Mwanampazi.


Alivitaja vijiji vilivyopo katika kata hiyo kuwa ni Mbalizi, Utngule, Idugumbi, Itimba, Iwala na Ihombe.

No comments:

Post a Comment