TAMASHA kubwa la muziki wa injili linalotarajiwa kufanyika
ukumbi wa Kanisa la Pentekoste Holiness Association Mission
(Makimbilio), karibu na lango kuu la Shule ya Sekondari Samora, Mbeya
Agosti 4, mwaka huu, linatarajiwa kuweka historia mpya.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa tamasha hilo, George
Kayala alisema kuwa, wasanii mbalimbali wa Bongo Movie wakiongozwa na
pacha wa muigizaji wa filamu na muziki, Husna Posh 'Dotnata', Dometria
Alphonce 'DD' wameandaa kitu kwa ajili ya wakazi wa Mbeya.
“Tamasha hilo litakuwa ni la kihistoria, kwani litapambwa na wasanii
wa filamu nchini wakiongozwa na pacha wa Dotnata na watakuwa na jambo la
kusema na watu watakaofika katika tamasha hilo,” alisema Kayala.
Kayala alisema kuwa tamasha hilo limeandaliwa na GMK Production kwa
ajili kuitambulisha albamu ya tatu ya ‘Nitang’ara Tu’ ya Mwinjilisti
Kabula George, ikiwa katika mfumo wa DVD na siku hiyo itauzwa kwa wakazi
wa Mbeya.
Kiingilio katika tamasha hilo ni sh 2,000 kwa watu wazima na 1,000 kwa
watoto na shughuli itaanza saa 7:00 mchana na kumalizika saa 12:00
jioni.
“Tumeamua kuweka kiingilio kidogo ili kila mmoja apate kuingia katika
tamasha hilo, ambalo litakuwa la kwanza kuwakutanisha nyota wa filamu na
waimbaji wa nyimbo za injili mkoani humo,” alisema Kayala.
Tamasha hilo limedhaminiwa na Ushindi Redio FM ya Mbeya, Shalom
Production, DD Entertainment, The Genesis Global College na Dotnata
Entertainment.
|
No comments:
Post a Comment