Mamlaka
ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), imesema ajira ya marubani wazalendo
ipo mashakani kwa sababu ndege nyingi nchini, zinaongozwa na wageni.TCAA
imesema hali hiyo imekuwa ikichangiwa na kampuni zinazotoa huduma hizo
nchini, kutumia ndege nyingi za kukodi zinazofanya kazi chini ya
masharti yanayotoa nafasi kubwa ya kuongozwa na marubani wa kigeni.(hd)