Pages

Saturday, 28 September 2013

Baraza la Usalama laidhinisha azimio kuhusu Syria


syria_UN_fb37a.jpg
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeidhinisha azimio jana Ijumaa(27.09.2013)ambalo linataka kuondolewa kabisa kwa silaha za sumu nchini Syria lakini halitishii kuchukuliwa hatia za kuiadhibu serikali ya rais Bashar al-Assad iwapo haitatekeleza.

Obama azungumza na Rouhani

130928014601_obama_rouhani_304x171_afp_57e39.jpg
Kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 30, viongozi wa Marekani na Iran wamezungumza moja kwa moja.

MSIGWA AMPONGEZA RAIS KIKWETE KWA MKAKATI WAKE WA KUPAMBANA NA UJANGILI

E84A9602_187c7.png
Na Francis Godwin Blog, Iringa
MBUNGE wa jimbo la Iringa mjini kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema)amempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa mkakati wake wa kunusuru vitendo vya ujangili katika hifadhi za Taifa.

Washtakiwa EPA jela miaka 13

Washtakiwa wa EPA, Bahati Mahenge (kulia), Manase Mwakale (katikati) wakiwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam jana, baada ya kuhukumiwa.Mahenge alihukumiwa kwenda jela miaka saba wakati Mwakale akihukumiwa miaka mitano. Picha na Venance Nestory 

Unyama wa Al-Shabaab wabainika ndani ya jengo

Mabaki ya jengo la Westgate lililoporomoka baada ya shambulizi la kigaidi jijini Nairobi, Kenya.Picha na Daily Mail 

Kwa ufupi
  • Taarifa zilizochapishwa na gazeti la Daily Mail la uingereza zikiwakariri wanausalama wa Kenya zinadai kuwa magaidi waliwatesa, kuwakata vidole, kuwanyofoa macho, kuwahasi wanaume na kisha kuwaning’iniza darini.

Kiama cha wauza unga chaja, faini kuondolewa, kifungo ni cha maisha

Madawa ya kulevya (Unga) yakiwa chini ya ulinzi 

Kwa ufupi
Sheria iliyopo sasa ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya ya mwaka 1995 (Sura ya 95, Ibara ya 16) inasema, endapo mtu atakamatwa kwa kosa la kumiliki, kusafirisha, kuzalisha au kutengeneza mashine ya dawa za kulevya, atahukumiwa kifungo cha maisha jela au kulipa faini ya Sh10 milioni.

Monday, 23 September 2013

ABIRIA ZAIDI YA 50 WANUSURIKA KIFO Iringa

ajali 7f5dd
Lori la Kampuni ya Ivory lililogongana uso kwa uso na Basi la Sai baba (HM)
ajali2 a0dc1
Askari wa usalama barabarani Iringa wakilitazama basi la kampuni ya Sai - baba Express lenye namba za Usajili T 668 BCD ambalo liligongana uso kwa uso na lori la kampuni ya Ivori lenye namba T 280 ADK eneo la Kibwabwa katika barabara kuu ya Mbeya - Iringa jana na watu zaidi ya watatu kujeruhiwa vibaya na wengine zaidi ya 50 ambao ni abiria wa basi hilo kunusurika kifo
ajali3 f85f7
Abiria waliokuwa kwenye basi la sai baba. Chanzo: Francis Godwin