Pages

Wednesday, 4 September 2013

MJANE WA MIAKA 60 ANAOMBA MSAADA WA KUTIBIWA MKONO WAKE ULIYOANZA KUHARIBIKA BAADA YA KUJERUHIWA NA NYOKA WILAYANI CHUNYA.


Mandela arudishwa nyumbani

Gari la kubebea wagonjwa likimrudisha nyumbani Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela jana
JOHANNESBURG, Afrika Kusini
SERIKALI ya Afrika Kusini imesema kuwa Rais wa zamani wa nchi hiyo, Nelson Mandela, ametolewa hospitali ambako amekuwa akitibiwa ugonjwa wa mapafu tangu Juni mwaka huu.

KESI DHIDI YA PINDA YAIVA

KESI ya kikatika iliyofunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) dhidi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, inatarajiwa kuanza kuunguruma Septemba 16, mwaka huu katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

NI KIAMA: ATAFUNWA USO NA MWAJIRI WAKE NYUMBANI

  • KABLA ALIANZA KUNG'ATA ULIMI WA MBWA

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mkazi wa Kijiji cha Nyabibuye Kakongo katika Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, Susuluka (16) anadaiwa kujeruhiwa vibaya usoni na bosi wake, Imani Paulo (36) kwa kung’atwa ng’atwa usoni na kisha kunyofolewa macho, pua na meno kubaki nje, kama ambavyo anaonekana pichani ukurasa wa mbele.

Mnigeria adakwa na dawa za kulevya Dar es Salaam

 
“Baada ya kumhoji ametueleza kuwa dawa hizo alizinunua maeneo ya Magomeni, kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya uchunguzi na mahojiano zaidi.” Clemence Jingu 

Rais Kikwete aongoza mazishi ya Askofu Kulola

Waziri Mkuu aliyejiuzulu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa jana wakati wa ibada ya mazishi ya Askofu Mkuu, Moses Kulola wa Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT) aliyezikwa nje ya Kanisa la Calvary

Museveni awakutanisha Rais Kikwete na Kagame

 
 

Kwa ufupi
Rais Kikwete alitoa ushauri huo wakati akiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU), zilizofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Mkutano wa leo utafanyika kwenye Ukumbi wa Commonwealth Resort, Munyonyo katikati ya Jiji la Kampala.

Dar es Salaam. 
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameitisha mkutano wa dharura wa marais wa nchi za Maziwa Makuu (ICGLR), kujadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa waalikwa kwenye mkutano huo ambao pia unatarajiwa kuhudhuriwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame.
Wakati hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikidhoofika, katika siku za karibuni, uhusiano wa Tanzania na Rwanda umekuwa wa shaka hasa baada ya Rais Kikwete kuishauri Serikali ya Rwanda kukaa na wapinzani ili kumaliza mzozo uliolikumba eneo la Maziwa Makuu.
Rais Kikwete alitoa ushauri huo wakati akiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU), zilizofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Mkutano wa leo utafanyika kwenye Ukumbi wa Commonwealth Resort, Munyonyo katikati ya Jiji la Kampala.
Kwa mujibu wa taarifa Rais Museveni ameitisha mkutano huo hasa kuzungumzia hatua ya Umoja wa Mataifa kupambana na Kundi la Waasi wa M23.
Mbali na viongozi hao wa Tanzania na Rwanda, viongozi wengine wanaotarajiwa kuhudhuria mkutano huo wanatoka Angola, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Sudan, na Zambia.