Pages
Wednesday, 4 September 2013
NI KIAMA: ATAFUNWA USO NA MWAJIRI WAKE NYUMBANI
- KABLA ALIANZA KUNG'ATA ULIMI WA MBWA
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mkazi wa
Kijiji cha Nyabibuye Kakongo katika Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, Susuluka
(16) anadaiwa kujeruhiwa vibaya usoni na bosi wake, Imani Paulo (36) kwa
kung’atwa ng’atwa usoni na kisha kunyofolewa macho, pua na meno kubaki nje,
kama ambavyo anaonekana pichani ukurasa wa mbele.
Rais Kikwete aongoza mazishi ya Askofu Kulola
Waziri Mkuu aliyejiuzulu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa
akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa jana wakati wa
ibada ya mazishi ya Askofu Mkuu, Moses Kulola wa Kanisa la Evangelist
Assemblies of God Tanzania (EAGT) aliyezikwa nje ya Kanisa la Calvary
Museveni awakutanisha Rais Kikwete na Kagame
Kwa ufupi
Rais Kikwete alitoa ushauri huo wakati akiwa katika
sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU),
zilizofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Mkutano wa leo utafanyika
kwenye Ukumbi wa Commonwealth Resort, Munyonyo katikati ya Jiji la
Kampala.
Dar es Salaam.
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameitisha mkutano wa dharura wa marais wa nchi za Maziwa Makuu (ICGLR), kujadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameitisha mkutano wa dharura wa marais wa nchi za Maziwa Makuu (ICGLR), kujadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa waalikwa
kwenye mkutano huo ambao pia unatarajiwa kuhudhuriwa na Rais wa Rwanda,
Paul Kagame.
Wakati hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo ikidhoofika, katika siku za karibuni, uhusiano wa
Tanzania na Rwanda umekuwa wa shaka hasa baada ya Rais Kikwete kuishauri
Serikali ya Rwanda kukaa na wapinzani ili kumaliza mzozo uliolikumba
eneo la Maziwa Makuu.
Rais Kikwete alitoa ushauri huo wakati akiwa
katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU),
zilizofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Mkutano wa leo utafanyika
kwenye Ukumbi wa Commonwealth Resort, Munyonyo katikati ya Jiji la
Kampala.
Kwa mujibu wa taarifa Rais Museveni ameitisha
mkutano huo hasa kuzungumzia hatua ya Umoja wa Mataifa kupambana na
Kundi la Waasi wa M23.
Mbali na viongozi hao wa Tanzania na Rwanda,
viongozi wengine wanaotarajiwa kuhudhuria mkutano huo wanatoka Angola,
Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Sudan, na Zambia.
Subscribe to:
Comments (Atom)

