Rwanda yajitetea kuhusu ushuru
Kwa ufupi
Ni ule wa kupandisha tozo za magari iliyopandishwa na nchi hiyo kwa madai ya kufanya ulinganifu
Dar es Salaam/Dodoma. Wakati ushuru wa magari
makubwa ukiwa umeshushwa kwa wiki moja, Serikali ya Rwanda imejitetea
ikisema haijafanya hujuma yoyote dhidi ya Tanzania, bali imepandisha
tozo hiyo ili kuifanya ilingane na ile inayolipwa Tanzania.
