Waziri wa Ujenzi Prof. Mbarawa afanya ziara ya kushtukiza KOJ Kurasini
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amemuagiza
Kaimu Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Nelson Mlali
kufanya uhakiki wa kampuni zinazotoa huduma mbalimbali bandarini ili
kuboresha utendaji kazi na kuepuka mgongano wa maslahi binafsi minongoni
wa watumishi wa bandari.



