Tanzania yapokea msaada wa shilingi bilioni 116.4 kutoka Japan.
Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini hati mbili za makubaliano
na Serikali ya Japan itakayoiwezesha Tanzania kupata kiasi Yen Bilioni 6
ambazo ni sawa na Sh. Bilioni 116.4 za Kitanzania.



