Rais Magufuli na Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya Raila Odinga Washiriki Misa Takatifu Pamoja Kwenye Kanisa Katoliki Chato
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye yupo
mapumzikoni nyumbani kwake Lubambangwe katika kijijini cha Mlimani,
Wilaya ya Chato Mkoani Geita, kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa
Rais, ameungana na waumini wenzake wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya
Chato, kusali ibada ya Jumapili ya Pili ya Pasaka ambapo pamoja na mambo
mengine amewahusia watanzania wote kuendelea kuliombea Taifa ili
liendelee kuwa na amani.




