Pages

Sunday, 3 April 2016

Rais Magufuli na Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya Raila Odinga Washiriki Misa Takatifu Pamoja Kwenye Kanisa Katoliki Chato 

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye yupo mapumzikoni nyumbani kwake Lubambangwe katika kijijini cha Mlimani, Wilaya ya Chato Mkoani Geita, kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais, ameungana na waumini wenzake wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato, kusali ibada ya Jumapili ya Pili ya Pasaka ambapo pamoja na mambo mengine amewahusia watanzania wote  kuendelea kuliombea Taifa ili liendelee kuwa na amani.

Rais Magufuli Atoa shilingi Milioni 10 nyumbani kwao Geita leo Kuchangia Upanuzi wa Kanisa 

 


Rais Magufuli ametoa mchango wa shilingi milioni 10 kwa kanisa la bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita kwa ajili kuchagia upanuzi wa kanisa hilo ambapo fedha hizo zimekabidhiwa na kaimu mnikulu Ngusa Samike katika misa ya pili ya ibada ya Jumapili ya pili ya Pasaka, iliyofanyika kanisani hapo leo tarehe 03 April, 2016.

Wednesday, 30 March 2016

Waziri wa Ujenzi Prof. Mbarawa afanya ziara ya kushtukiza KOJ Kurasini 

 


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amemuagiza Kaimu Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Nelson Mlali kufanya uhakiki wa kampuni zinazotoa huduma mbalimbali bandarini ili kuboresha utendaji kazi na kuepuka mgongano wa maslahi binafsi minongoni wa watumishi wa bandari.

Tanzania yapokea msaada wa shilingi bilioni 116.4 kutoka Japan. 

 

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini hati mbili za makubaliano na Serikali ya Japan itakayoiwezesha Tanzania kupata kiasi Yen Bilioni 6 ambazo ni sawa na Sh. Bilioni 116.4 za Kitanzania.

Tuesday, 29 March 2016

Auawa Kwa Kuchomwa Kisu Akigombea Mwanamke Baa 

 


Watu  wawili wameuawa mkoani Shinyanga katika matukio mawili tofauti, likiwamo la kijana kuchomwa kisu akigombea mwanamke katika baa ya Matunu mjini Shinyanga.

Askari wa Zimamoto Wanusurika Kupigwa Baada ya Kuchelewa Kufika Eneo la Tukio

 

Askari wa Kikosi cha Zimamoto, Manispaa ya Shinyanga wamenusurika kipigo kutoka kwa wananchi wa mtaa wa Banduka, kata ya Ndala mjini hapa, baada ya kuchelewa kufika kwenye tukio la nyumba kuungua moto ikiwa na watoto ndani yake.

Rais Magufuli Atoa Hati Ya Kiwanja Chenya Ukubwa wa Hekari 5 Kwa Bohari Ya Dawa (MSD) 

 

RAIS Dk. John Magufuli kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametoa kiwanja chenye ukubwa wa ekari 5 kwa Bohari ya Dawa (MSD) kilichopo Luguluni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, kwa ajili ya ujenzi wa Bohari ya Dawa ili kuondoa upotevu wa fedha kwa maghala ya kukodi.