Pages

Tuesday, 29 March 2016

Rais Magufuli Atoa Hati Ya Kiwanja Chenya Ukubwa wa Hekari 5 Kwa Bohari Ya Dawa (MSD) 

 

RAIS Dk. John Magufuli kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametoa kiwanja chenye ukubwa wa ekari 5 kwa Bohari ya Dawa (MSD) kilichopo Luguluni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, kwa ajili ya ujenzi wa Bohari ya Dawa ili kuondoa upotevu wa fedha kwa maghala ya kukodi.

Watu Wanne Watiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kutumia Jina la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Kutapeli 

 


Watu wanne wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na tuhuma za kujipatia fedha kwa kutumia jina la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Kamati ya Bunge Yamchokonoa Rais Magufuli Kuhusu Vibali vya Sukari 

 


KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, imemwomba Rais John Magufuli kuangalia tatizo la uhaba wa sukari nchini na kuona jinsi ya kufanya kuruhusu kutoa vibali kwa wafanyabiashara kuagiza sukari nje ya nchi.

Wafanyakazi watatu TANESCO Watiwa Mbaroni Kufuatia Kifo cha Mfanyakazi Mwenzao Aliyenaswa na Umeme Juu ya Nguzo 

 


Wafanyakazi watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Morogoro, wanashikiliwa na Polisi wakihojiwa kutokana na kifo cha mfanyakazi mwenzao, Deo Elias (30), mkazi wa Mazimbu, Manispaa ya Morogoro kwa kunaswa na umeme juu ya nguzo.

Diwani wa CHADEMA Apeta Mahakamani, wa CCM Chali baada ya Pingamizi Lake Kutupwa 

 


Mahakama  ya Hakimu Mkazi Arusha imetupilia mbali kesi ya kupinga matokeo ya udiwani katika kata ya Musa wilayani Arumeru Magharibi iliyofunguliwa na mgombea wa CCM, Flora Zelote dhidi ya diwani wa Chadema, Loth Laizer.

Monday, 28 March 2016

20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ Aliyemgonga Mtembea Kwa Miguu 

 


Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu.

Rais Magufuli Amuapisha Mkuu Wa Mkoa Mpya Wa Songwe Mhe. Chiku Gallawa Ikulu Dar Es Salaam