Wafanyakazi watatu TANESCO Watiwa Mbaroni Kufuatia Kifo cha Mfanyakazi Mwenzao Aliyenaswa na Umeme Juu ya Nguzo
Wafanyakazi watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Morogoro,
wanashikiliwa na Polisi wakihojiwa kutokana na kifo cha mfanyakazi
mwenzao, Deo Elias (30), mkazi wa Mazimbu, Manispaa ya Morogoro kwa
kunaswa na umeme juu ya nguzo.





