20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ Aliyemgonga Mtembea Kwa Miguu
Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya
Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania
(JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa
akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu.



