Pages

Sunday, 3 April 2016

Vigogo NHC na EWURA Wakana Kulipwa Mhashara wa Milioni 36 kwa Mwezi 

 


Mabosi  wa mashirika mawili ya Serikali nchini, wanaodaiwa kulipwa mshahara wa Sh milioni 36, wamekanusha madai hayo, huku wakielezea kushangazwa na taarifa hizo wakati hata nusu ya fedha hizo, hawapati.

Ndoo Walizobeba Kigogo wa Zamani wa TRA na Miss Tanzania Wakati Wakipelekwa Gerezani Zaibua Utata 

 

Kitendo cha aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya pamoja na maofisa wawili waandamizi wa zamani wa Benki ya Stanbic, Tawi la Tanzania, Sioi Solomoni na Shose Sinare kubeba ndoo wakati wakitoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuelekea mahabusu, kimezua maswali mengi.

Rais Magufuli na Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya Raila Odinga Washiriki Misa Takatifu Pamoja Kwenye Kanisa Katoliki Chato 

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye yupo mapumzikoni nyumbani kwake Lubambangwe katika kijijini cha Mlimani, Wilaya ya Chato Mkoani Geita, kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais, ameungana na waumini wenzake wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato, kusali ibada ya Jumapili ya Pili ya Pasaka ambapo pamoja na mambo mengine amewahusia watanzania wote  kuendelea kuliombea Taifa ili liendelee kuwa na amani.

Rais Magufuli Atoa shilingi Milioni 10 nyumbani kwao Geita leo Kuchangia Upanuzi wa Kanisa 

 


Rais Magufuli ametoa mchango wa shilingi milioni 10 kwa kanisa la bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita kwa ajili kuchagia upanuzi wa kanisa hilo ambapo fedha hizo zimekabidhiwa na kaimu mnikulu Ngusa Samike katika misa ya pili ya ibada ya Jumapili ya pili ya Pasaka, iliyofanyika kanisani hapo leo tarehe 03 April, 2016.

Wednesday, 30 March 2016

Waziri wa Ujenzi Prof. Mbarawa afanya ziara ya kushtukiza KOJ Kurasini 

 


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amemuagiza Kaimu Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Nelson Mlali kufanya uhakiki wa kampuni zinazotoa huduma mbalimbali bandarini ili kuboresha utendaji kazi na kuepuka mgongano wa maslahi binafsi minongoni wa watumishi wa bandari.

Tanzania yapokea msaada wa shilingi bilioni 116.4 kutoka Japan. 

 

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini hati mbili za makubaliano na Serikali ya Japan itakayoiwezesha Tanzania kupata kiasi Yen Bilioni 6 ambazo ni sawa na Sh. Bilioni 116.4 za Kitanzania.

Tuesday, 29 March 2016

Auawa Kwa Kuchomwa Kisu Akigombea Mwanamke Baa 

 


Watu  wawili wameuawa mkoani Shinyanga katika matukio mawili tofauti, likiwamo la kijana kuchomwa kisu akigombea mwanamke katika baa ya Matunu mjini Shinyanga.

Askari wa Zimamoto Wanusurika Kupigwa Baada ya Kuchelewa Kufika Eneo la Tukio

 

Askari wa Kikosi cha Zimamoto, Manispaa ya Shinyanga wamenusurika kipigo kutoka kwa wananchi wa mtaa wa Banduka, kata ya Ndala mjini hapa, baada ya kuchelewa kufika kwenye tukio la nyumba kuungua moto ikiwa na watoto ndani yake.

Rais Magufuli Atoa Hati Ya Kiwanja Chenya Ukubwa wa Hekari 5 Kwa Bohari Ya Dawa (MSD) 

 

RAIS Dk. John Magufuli kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametoa kiwanja chenye ukubwa wa ekari 5 kwa Bohari ya Dawa (MSD) kilichopo Luguluni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, kwa ajili ya ujenzi wa Bohari ya Dawa ili kuondoa upotevu wa fedha kwa maghala ya kukodi.

Watu Wanne Watiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kutumia Jina la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Kutapeli 

 


Watu wanne wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na tuhuma za kujipatia fedha kwa kutumia jina la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Kamati ya Bunge Yamchokonoa Rais Magufuli Kuhusu Vibali vya Sukari 

 


KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, imemwomba Rais John Magufuli kuangalia tatizo la uhaba wa sukari nchini na kuona jinsi ya kufanya kuruhusu kutoa vibali kwa wafanyabiashara kuagiza sukari nje ya nchi.

Wafanyakazi watatu TANESCO Watiwa Mbaroni Kufuatia Kifo cha Mfanyakazi Mwenzao Aliyenaswa na Umeme Juu ya Nguzo 

 


Wafanyakazi watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Morogoro, wanashikiliwa na Polisi wakihojiwa kutokana na kifo cha mfanyakazi mwenzao, Deo Elias (30), mkazi wa Mazimbu, Manispaa ya Morogoro kwa kunaswa na umeme juu ya nguzo.

Diwani wa CHADEMA Apeta Mahakamani, wa CCM Chali baada ya Pingamizi Lake Kutupwa 

 


Mahakama  ya Hakimu Mkazi Arusha imetupilia mbali kesi ya kupinga matokeo ya udiwani katika kata ya Musa wilayani Arumeru Magharibi iliyofunguliwa na mgombea wa CCM, Flora Zelote dhidi ya diwani wa Chadema, Loth Laizer.

Monday, 28 March 2016

20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ Aliyemgonga Mtembea Kwa Miguu 

 


Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu.

Rais Magufuli Amuapisha Mkuu Wa Mkoa Mpya Wa Songwe Mhe. Chiku Gallawa Ikulu Dar Es Salaam 


RADHI

TUNAOMBA RADHI KWANI TUPO KWENYE MAREKEBISHO ILI KUBORESHA UTOAJI WA HUDUMA ZETU, ENDELEA KUTUFUATILIA. BY MWANGA WA JAMII BLOGSPORT

Sunday, 27 March 2016

Rais Magufuli aitakia heri Taifa Stars dhidi ya Chad 

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameitakia heri timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) katika mchezo wake dhidi ya Timu ya Taifa ya Chad, utakaofanyika katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam, kesho tarehe 28 Machi, 2016. 

Rais Magufuli Awataka Watanzania kuwa Wamoja 

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasihi watanzania kuendelea kuwa wamoja na kushirikiana kuijenga nchi yao, badala ya kubaguana.

Serikali Yaanda Muongozo wa Ajira kwa Vijana 

 

Kutokana na Tanzania kuwa na uchumi wa soko huria vijana wengi wameanza kushiriki katika sekta isiyo rasmi hivyo kunawafanya kuchangia nusu ya uchumi wa Taifa katika shughuli zao za kila siku.

Tuesday, 19 January 2016