Pages
▼
Sunday, 3 April 2016
Ndoo Walizobeba Kigogo wa Zamani wa TRA na Miss Tanzania Wakati Wakipelekwa Gerezani Zaibua Utata
Kitendo
cha aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry
Kitilya pamoja na maofisa wawili waandamizi wa zamani wa Benki ya
Stanbic, Tawi la Tanzania, Sioi Solomoni na Shose Sinare kubeba ndoo
wakati wakitoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuelekea mahabusu,
kimezua maswali mengi.
Rais Magufuli na Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya Raila Odinga Washiriki Misa Takatifu Pamoja Kwenye Kanisa Katoliki Chato
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye yupo
mapumzikoni nyumbani kwake Lubambangwe katika kijijini cha Mlimani,
Wilaya ya Chato Mkoani Geita, kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa
Rais, ameungana na waumini wenzake wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya
Chato, kusali ibada ya Jumapili ya Pili ya Pasaka ambapo pamoja na mambo
mengine amewahusia watanzania wote kuendelea kuliombea Taifa ili
liendelee kuwa na amani.
Rais Magufuli Atoa shilingi Milioni 10 nyumbani kwao Geita leo Kuchangia Upanuzi wa Kanisa
Rais
Magufuli ametoa mchango wa shilingi milioni 10 kwa kanisa la bikira
Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita kwa ajili kuchagia upanuzi wa kanisa
hilo ambapo fedha hizo zimekabidhiwa na kaimu mnikulu Ngusa Samike
katika misa ya pili ya ibada ya Jumapili ya pili ya Pasaka, iliyofanyika
kanisani hapo leo tarehe 03 April, 2016.
Wednesday, 30 March 2016
Waziri wa Ujenzi Prof. Mbarawa afanya ziara ya kushtukiza KOJ Kurasini
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amemuagiza
Kaimu Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Nelson Mlali
kufanya uhakiki wa kampuni zinazotoa huduma mbalimbali bandarini ili
kuboresha utendaji kazi na kuepuka mgongano wa maslahi binafsi minongoni
wa watumishi wa bandari.
Tanzania yapokea msaada wa shilingi bilioni 116.4 kutoka Japan.
Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini hati mbili za makubaliano
na Serikali ya Japan itakayoiwezesha Tanzania kupata kiasi Yen Bilioni 6
ambazo ni sawa na Sh. Bilioni 116.4 za Kitanzania.
Askari wa Zimamoto Wanusurika Kupigwa Baada ya Kuchelewa Kufika Eneo la Tukio
Askari
wa Kikosi cha Zimamoto, Manispaa ya Shinyanga wamenusurika kipigo
kutoka kwa wananchi wa mtaa wa Banduka, kata ya Ndala mjini hapa, baada
ya kuchelewa kufika kwenye tukio la nyumba kuungua moto ikiwa na watoto
ndani yake.
Rais Magufuli Atoa Hati Ya Kiwanja Chenya Ukubwa wa Hekari 5 Kwa Bohari Ya Dawa (MSD)
RAIS
Dk. John Magufuli kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
ametoa kiwanja chenye ukubwa wa ekari 5 kwa Bohari ya Dawa (MSD)
kilichopo Luguluni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, kwa ajili ya
ujenzi wa Bohari ya Dawa ili kuondoa upotevu wa fedha kwa maghala ya
kukodi.
Wafanyakazi watatu TANESCO Watiwa Mbaroni Kufuatia Kifo cha Mfanyakazi Mwenzao Aliyenaswa na Umeme Juu ya Nguzo
Wafanyakazi watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Morogoro,
wanashikiliwa na Polisi wakihojiwa kutokana na kifo cha mfanyakazi
mwenzao, Deo Elias (30), mkazi wa Mazimbu, Manispaa ya Morogoro kwa
kunaswa na umeme juu ya nguzo.
Monday, 28 March 2016
20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ Aliyemgonga Mtembea Kwa Miguu
Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya
Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania
(JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa
akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu.
RADHI
TUNAOMBA RADHI KWANI TUPO KWENYE MAREKEBISHO ILI KUBORESHA UTOAJI WA HUDUMA ZETU, ENDELEA KUTUFUATILIA. BY MWANGA WA JAMII BLOGSPORT













